CHOBA
KILA BINADAMU NI MKONO WA MUNGU WA KUPITISHIA BARAKA KWA MWINGINE
Kijana Choba akiwa kwenye mhangaiko ya uhutaji akakutana na Mzee Juma aliyempa chai na sehemu ya kujenga kibanda. Zaidi mno wote wawili wakaamua kuishi pamoja kila mmoja kumwondolea mwenzake upweke. Tokea hapo zikawatokea baraka zilizowafanya kuwa watu wenye nacho. Na kama haikutosha Choba akaishia kuwa mkwe kwa Mzee Juma kwa kumwoa Jesca binti Juma.
Bonge baada ya kukutana na maangamizi yaliyowakumba wazazi wake na jamaa walioishi nao, alihisaniwa na mkuu wa Chuo alikosoma ambaye aliichukua nafasi ya mzazi na mafadhili kwa mwathirika huyu. Urithi alioachiwa Bonge akautumia vyema kwa kuwaendeleza Choban a Jesca binti Juma katika elimu aliyowawezesha kuchukua nafasi za juu za ajiria katika miradi aliyoanzisha.
CHOBEMICO, Kampuni ya madini iliyoasisiwa na Choba na Benson (Bonge) imekuwa chombo cha ukombozi wa yatima hawa na mwendelezo wa wale wote waliokuwa na mahusiano nao. Zaidi mno ilisaidia kumpatia Choba mke mwema na sherehe ya harusi iliyokuwa na karamu kubwa ya kimataifa
Sold by: Lackson Tungaraza
Sold by: Godfrey Ngaleya
Sold by: Lackson Tungaraza
Sold by: Lackson Tungaraza