
OFISI NA KARAMA YA UNABII KATIKATI YA MWILI WA KRISTO JUU YA NCHI
Ofisi na karama ya Unabii ndani ya Mwili wa Kristo ni ofisi ya Upatanisho; Haiishii tu katika kusikia, kuona na kusema bali ni kuupatanisha ulimwengu na Mungu kupitia Yesu Kristo, kama ambavyo Mungu Mwenyewe alitupatanisha naye kupitia nafsi yake ambaye ni KRISTO.
Taifa la Pete Ya Muhuri ni Kanisa la Bwana Yesu Kristo, tuliopewa Ujumbe wa Uana na Ufalme wa Mungu kuuhubiri kwa mataifa duniani ili Wana wazaliwe, kujaza nchi, kuongezeka, kutiisha na kutawala pamoja na Kristo sasa na miaka elfu ijayo.
Kupitia Ujumbe huu tunang’oa, kubomoa, kuharibu, kuangamiza, ili kujenga na kupanda.
Karibu sana katika kitabu hiki cha OFISI NA KARAMA YA UNABII KATIKA MWILI WA KRISTO JUU YA NCHI sehemu ya kwanza.
Tarajia sehemu ya pili.