Falsafa Ya Uchumi Wa Mawazo
Falsafa Ya Uchumi Wa Mawazo
Nguvu kubwa kuliko zote aliyopewa mwanadamu ni nguvu ya wazo: Sio nguvu ya mwili, fedha wala mamlaka. Mwanadamu hutawaliwa na kile anachokiamini, huongozwa na kile anachokifikiri na hujengwa na kile anachokiruhusu kikae ndani ya akili yake. Kila mabadiliko makubwa yaliyowahi kutokea duniani yalitanguliwa na wazo. Kila ustaarabu, uvumbuzi, mafanikio na mapinduzi ya maendeleo yalizaliwa kwanza katika ufahamu wa mtu mmoja kabla hayajawa sehemu ya historia. Wazo ni zaidi ya fikra ya kawaida. Wazo ni mbegu ya uhalisia, mwanzo wa kile ambacho bado hakijaonekana, daraja linalounganisha ulimwengu wa uwezekano na ulimwengu wa matokeo. Mwanadamu huishi mara mbili: ndani ya mawazo yake na ndani ya matokeo ya mawazo hayo. Ndiyo maana tofauti kati ya watu mara nyingi haipo katika mazingira wanayoishi bali ipo katika mawazo wanayoyabeba. Watu wawili wanaweza kusimama mahali pamoja, wakaona jambo lile lile lakini mmoja akaona mwisho na mwingine akaona mwanzo, mmoja akaona tatizo na mwingine akaona fursa na mmoja akaona kikwazo na mwingine akaona njia. Hapo ndipo siri ya mafanikio ilipo.
Sold by: Lackson Tungaraza
Sold by: Lackson Tungaraza
Sold by: Lackson Tungaraza