MAISHA NA FALSAFA ZA SAFARI
“Maisha na Falsafa za Safari,” ni kitabu kinachoelezea safari ya maisha, changamoto mbalimbali, elimu, maarifa, ujuzi, uzoefu, kuhamasisha na kujengeana mitazamo chanya ya kukabili mambo na kusonga mbele katika kupambana kimaisha kwa matokeo chanya katika Ulimwengu huu wa kimwili na kiroho. Kitabu hiki kimegusia mambo mbalimbali katika safari hiyo, kama vile jinsi mwanadamu anavyosafiri katika safari hiyo, kuanzia kuzaliwa na kuja hapa duniani, utoto wake, kukua na ujana wake, mpaka anafikia uzeeni na kunyauka, pia changamoto mbalimbali anazokutana nazo kimaisha, imani, uchumi, ujasiriamali, utawala, maadili, malezi, makuzi, mahusiano, falsafa, elimu, ujuzi, majibu, hamasa na namna anavyokabili mazingira yake na jamii kwa ujumla.
“Maisha ni mafupi, ila yana safari ndefu ndani yake.”
“Maisha na Falsafa za Safari,” ni kitabu kinachoelezea safari ya maisha, changamoto mbalimbali, elimu, maarifa, ujuzi, uzoefu, kuhamasisha na kujengeana mitazamo chanya ya kukabili mambo na kusonga mbele katika kupambana kimaisha kwa matokeo chanya katika Ulimwengu huu wa kimwili na kiroho.
Kama ilivyo, maisha ni mafupi kwa namna ya muda tuliowekewa kuishi hapa duniani na namna ya mambo yaliyopo yanavyotukabili na kutupasa kuyatimiza kwa wakati. Wengine hudiriki kusema kuwa, “Muda hautoshi,” hasa kwa wale wengi walio na matumaini; yaani mambo ni mengi, lakini muda ni mchache huku tukizidi kunyauka.
Ila pia, pamoja na ufupi huo wa maisha, lakini ukija kuangalia namna ya baadhi ya mambo yalivyo magumu, pamoja na changamoto na mataabiko yaliyopo kwa baadhi ya watu, hufanya safari hii kwa wengine kuonekana ni ndefu sana, tena yenye dhiki na mataabiko, na kufikia kusema kuwa, “Muda hauendi, dunia imesimama na kuwaelemea,” hasa kwa wale waliokata tamaa na kupoteza matumaini.
Kitabu hiki kimegusia mambo mbalimbali katika safari hiyo, kama vile jinsi mwanadamu anavyosafiri katika safari hiyo, kuanzia kuzaliwa na kuja hapa duniani, utoto wake, kukua na ujana wake, mpaka anafikia uzeeni na kunyauka, pia changamoto mbalimbali anazokutana nazo kimaisha, imani, uchumi, ujasiriamali, utawala, maadili, malezi, makuzi, mahusiano, falsafa, elimu, ujuzi, majibu, hamasa na namna anavyokabili mazingira yake na jamii kwa ujumla.
Ni maneno yenye kufunza, kutoa elimu, maarifa, hekima, ujuzi, falsafa mbalimbali, kuhamasisha, kutia moyo na kutupatia ufunuo, taswira na dira mpya kimtazamo katika kukabiliana na mazingira yetu kimaisha, na kisha kusimama imara na kusonga mbele.