
NGUVU YA PASAKA
KATIKA KUSHINDA VITA YA KIROHO.
Mungu aliupenda sana ulimwengu hata akaamua kumtoa mwana wake wa pekee YESU KRISTO kama dhamana ya dhambi zetu sisi wanadamu ili tupone. Lakini mpango huu wa Mungu umekuwa ukipingwa na shetani usitimie kwenye maisha ya watu wengi hasa wakristo. Hivyo shetani amekuwa anashambulia kwa njia mbali mbali mpango huo hapa duniani ili kuzuia usitimie kama ambavyo Mungu alivyokusudia.
Ukweli ni kuwa mapambano katika vita ya kiroho ni nguvu za giza chini ya shetani na washirika wake dhidi ya nguvu za nuru chini ya Yesu Kristo. Pamoja na ukweli huo wa mashambulizi ya shetani yanayokuja kwa njia mbali mbali lakini Mungu amewapa watu wake hasa wakristo silaha nyingi za kumshambulia na kujilinda dhidi ya mashambulizi hayo.
Sasa changamoto kubwa kwa watu wengi huwa sio mashambulizi ya shetani bali ufahamu na uelewa wa vita hii na namna mbali mbali ya kutumia silaha ya nguvu ya Pasaka katika kushambulia na kujilinda. Nimeandika kitabu hiki kwa malengo ya kuweka MUONGOZO na DIRA kwa kila mtu hasa mkristo mwenye nia ya kutaka kujifunza na kuzijua siri hizi za mapigano ya vita za kiroho ili aweze kujitegemea katika mapambano mbali mbali dhidi ya shetani.
HIVYO BASI...
Kitabu hiki kinampatia mtu yoyote yule hasa mkristo kuwa na ufahamu wenye utayari wa namna ya kumjua adui katika ulimwengu wa roho, maana na uhalisia mpana zaidi wa vita ya kiroho, utambuzi wa silaha mchanganyiko zinazohitajika kutumika katika vita ya kiroho na siri nyingi zilizomo katika kutumia nguvu ya silaha ya Pasaka katika kujihakikishia ushindi katika vita hii ya kiroho.
Sold by: Lackson Tungaraza
Sold by: Lackson Tungaraza