
UKWELI WA MAISHA
Je, unaishi ili kutimiza kusudi la maisha yako au unatimiza kusudi la maisha yako ili uishi?
NAJUA utakuwa umeshawahi kujiuliza kuhusu maisha ni nini? Kwa nini kuna kuishi ndani ya maisha yenyewe? Majibu yake ndio yakanifanya niandike kitabu hiki ambacho kitaweka usawa na ukweli wa kuishi katika mchakato wenyewe wa maisha. Hii imetokana na maisha ya mazoea ambayo watu wengi wamekuwa wakiishi, kimsingi siku za hivi karibuni kumekuwa na IDADI kubwa ya watu wengi kupata changamoto ya AFYA YA AKILI kutokana na CHANGAMOTO za maisha. Je, ni kweli maisha yamekuwa na changamoto kubwa kiasi hicho hadi kufikia watu wengi kujiua? Baada ya kutafakari sana nikaona nikuandikie habari za UKWELI WA MAISHA ili walau uchukue tahadhari mapema pindi unapokumbana na changamoto za MAISHA.
Sikiliza nikwambie changamoto katika maisha ni kitu cha kawaida, na zimekuwepo toka vizazi hadi vizazi lakini tatizo kubwa ni pale changamoto hizo zinapopelekea watu wapate matatizo ya AKILI na wengine wajiue. Sio kwamba wazazi wetu walikuwa hawana changamoto katika maisha yao, walikuwa nazo kwa sababu changamoto za maisha zimekuwepo lakini mbona wao walikuwa hawajiui wala kupata matatizo ya afya ya akili kama sisi vijana wa siku hizi tunavyofanya? Wazazi wetu waliijua misingi inayojenga ukweli wa maisha kwa kufanya uchunguzi wa kina kuhusu SABABU na MATOKEO.
Hivyo basi ni tumaini langu kitabu hiki kitakupa mwongozo wa kuelewa kuhusu safari yako ya maisha, kwa sababu mengi yaliyoandikwa humu yanaakisi uhalisia wa maisha ya wa watu wengi. Tukumbuke kuwa kuishi katika kusudi lako ni mpango halisi kabisa wa Mungu kwa wanadamu, hivyo tusiufanye kuwa mpango wa shetani kwa KUJITAHIDI KUISHI.
Sold by: Lackson Tungaraza
Sold by: Lackson Tungaraza