U BINTI WA NANI WEWE?
Namna Binti Anavyoweza Kuishi Maisha Ya Ushindi Na Mguso Chanya Kwa Jamii Inayomzunguka Na Dunia Kwa Ujumla
Katika Karne Hii Ya 21, Unawezaje Kuwa Binti Mwenye Maisha Ya Ushindi Dhidi Ya Dhambi Na Ushawishi Mkubwa Wa Kuangukia Upotevuni?
Unawezaje Kuishi Maisha MATAKATIFU Katikati Ya Dunia Hii Iliyojaa Kila Aina Ya Mitego Na Ushawishi Wa Kukuangushia Maovuni?
Unawezaje Kuwa Binti Mwenye Maisha Yenye Mvuto Na Ushawishi Chanya Kwa Jamii Yako Na Dunia Hii Katikati Ya Zamani Hizi Zilizopotoka?
Unawezaje Kutengeneza Maisha Yenye Uthamani Kiasi Cha Kufanikiwa Kuwa Kielelezo Kwa Jamii Yako Na Dunia Kwa Ujumla?
Haya Ni Maswali Muhimu Ambayo Inawezekana Umekuwa Ukijiuliza, Na Hata Kama Hujawahi Kujiuliza; Basi Majibu Ya Maswali Haya Na Mengine Mengi Yameachiliwa Ndani Ya Kitabu Hiki Kwa Msaada Wa Roho Mtakatifu.
Mithali 4:7
[7]Bora hekima, basi jipatie hekima; Naam, kwa mapato yako yote jipatie ufahamu.
Maandiko Yanatutaka Kwa Gharama Zetu Ikiwezekana Zote Tujipatie Ufahamu, Kwanini TUTUMIE Gharama Kujipatia Ufahamu?
Mithali 11:9
[9]Asiyemcha Mungu humpoteza jirani yake kwa kinywa chake; Bali wenye haki watapona kwa maarifa.
Maandiko Yanatujibu Swali Hili Muhimu Sana, Wenye Haki Watapona Kwa Maarifa! Tunaishi Kwenye Dunia Ambayo Kwa Gharama Zozote Unapaswa Kutafuta Maarifa Sahihi Yatakayokusaidia Uishi Maisha Ya Ushindi, Uthamani, Utofauti, Mguso Chanya Kiasi Cha Dunia Kukuuliza U Binti Wa Nani Wewe..
Kitabu Kimebeba Sehemu Ya Maarifa Yanayotokana Na Ufunuo Wa Roho Mtakatifu Kutokea Kwenye Neno La Mungu, Na Maarifa Haya Yatakusaidia Na Kukuwezesha Kuwa Binti Mwenye Maisha Ya Ushindi, Uthamani, Utofauti Na Mguso Chanya Kwa Jamii Inayokuzunguka Na Dunia Kwa Ujumla!
Mwanzo 24:23
[23]akasema, U binti wa nani wewe? Tafadhali uniambie. Je! Iko nafasi katika nyumba ya baba yako tupate mahali pa kukaa kwa muda?
U Binti Wa Nani Wewe?
Karibu Ujipatie Nakala Yako Sasa..!