
MUONGOZO WA MAOMBI YA KUFUNGA YA SIKU 70
Kuja kwako” (Zab 65:2). rnTunamshukuru Mungu kwa yale ambayo amekuwa akifanya kila tusimamapo mbele zake na kila tumuombapo. Mungu ametupa utaratibu wa maombi ya kufunga kwa siku 70 kila siku masaa 12 ili kuwasha moto wa uamsho kwa kuruhusu mtembeo wa Roho ya uamsho ndani ya kanisa lake. rnSiku 70 za matendo makuu ya Mungu, kuzalisha mashujaa wengi wa maombi, kufungua milango mingi ya Baraka kwaajili ya watu wa Mungu, kuharibu utendajikazi wa nguvu za giza katika maisha ya wengi, kuzuia uharibifu uliopo na utakaokuja kwenye maisha ya watu, kupindua wamiliki wa anga na malango ya miji, kuizaa Tanzania mpya kwa maombi, kuinuka kwa nguvu kubwa za Mungu ili kumiliki na kutawala, n.krnMaombi yana thamani kubwa sana kwenye maisha ya mkiristo mwenye uhai, Maombi ni hitaji sio chaguo. Maandiko yanasema; rnMATHAYO 17:21 rn“Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.” rnMilima mingine haitaanguka isipokuwa imeshambuliwa na mizinga ya maombi ya kufunga.
Hakutakuwa na matokeo ikiwa hakuna madhabahu ya maombi, Maombi ndio pumzi ya mkristo pale anapotaka kuendelea kuwa hai katika imani yake.
Kitabu hiki kinatoa Muongozo wa maombi ya kufunga ya siku 70, Kinatoa muongozo wa mahitaji na maombi pamoja na maandiko ya kusimamia wakati wa maombi.